Pages

Wednesday, May 9, 2012

**UJUMBE MZITO KWA BAADHI YA VITUO VYA REDIO MKOANI MBEYA**

Habari!!
Mmiliki wa Blogu zifuatazo KAMANGA NA MATUKIO na KAMANGA na INJILI ambaye pia ni Mwandishi wa habari wa Kituo cha redio Bomba FM, anatoa onyo kwa baadi ya Vituo vya habari mkoani Mbeya ambavyo hujimilikisha habari zake na kudai kuwa kwa mujibu wa uchunguzi wa waandishi wao ndio wamefanikisha upatikanaji wa habari hizo na badala yake wamekuwa wakikaa maofisini mwao na kunakili. Hivyo basi anaombeni kubadilisha kauli hizo kabla ya mwanasheria wake hajachukua hatua.

Anamalizia kwa kusema Tushirikiane na Tutendeane haki juu ya hizo habari kwa kuhabarisha jamii.
 
Ezekiel Richard Kamanga.
Mbeya Tz.
 +255754 490 752
 +255787 490 752

NDUGU WA USUSIA MWILI WA MAREHEMU KWA SIKU MBILI, KUTOWATEMBELEA NDUGUZE NDO CHANZO MASKINI MAUMIVU YA NONDO YAMSABABISHIA KIFO.

*Wadai marehenu hakuwajali.
*Mwili washinda ndani ndugu watokomea.
*Balozi wa mtaa aokoa jahazi.
******
Habari kamili na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Familia ya Edson Mbembela wa Nzovwe imejikuta ikiingia matatani baada ya kuutelekeza mwili wa ndugu yao aliyekuwa mjane ambaye aliolewa na mwanawe Ebnesa Mbembela aliyefariki mwaka 2005.

Marehemu alikuwa akiishi mtaa wa Iyela jijini Mbeya na kufariki Mei 7 mwaka huu majira ya saa nene mchana katika nyumba inayomilikiwa na Bwana Giseon Kyebeleka, ambaye ni Askari magereza wa Chuo cha Magereza Kiwira mkoani Mbeya.

Aidha inadaiwa marehemu alifariki kutokana na maumivu ya kichwa kutokana na kupiga nondo hivi eneo la Sido jijini hapa alipokuwa anarejea nyumbani majira ya usiku.

Balozi wa Mtaa huo Bwana Lwitiko Mwanyingili amesema marehemu alijaaliwa kupata watoto wanne, ambapo wawili walikuwa wakiishi na marehemu kabla ya kifo chake na mara baada ya kufariki walimtafuta baba mkwe Bwana Edson Mbembela na kumtaarifu juu ya kifo cha mkwewe.

Baada ya taarifa hizo Bwana Mbembela na mkewe Bi Maria Mbembela (70) walidai hawako tayari kuzika kwa vile marehemu hakumuuguza marehemu mmewe aliyefariki mwaka 2005 na pia alikuwa hawatembelei nyumbani.

Aidha Baba mkwe huyo aliagiza ndugu wa marehemu huyo wamzike na baada ya mazishi aletewe watoto hao kwa ajili ya kuwatunza.

Uapnde wa pili wa ndugu wa marehemu nao walikataa kumzika wakidai kuwa binti yao walimuoza kwa ukoo wa Mbembela na pia marehemu alikuwa hawatembelei hivyo hawana haki ya kumzika.

Balozi Mwanyingili aliamua kumtaarifu Mwenyekiti wa mtaa wa Iyela Bwana Japhet Mwangonele ambapo alizikutanisha pande zote mbili bila mafanikio na hata alipotoa taarifa Kituo cha Polisi Mwanjelwa nao hawakuwa nala kufanya.

Naye, Mchungaji wa Kanisa la Church of God Solomon Mwashoma, amesema amesikitishwa sana na tukio hilo na kumhukumu marehemu kwani huo ni ukatili.

Mchungaji huyo ameenda mbali sana kwa kusema si vema kuwanyanyasa wajane na hii ni hatari zaidi kwa jamii ya kitanzania na kuwaasa watu wenye tabia kama hizo kuacha mara moja.

Pia viongozi mbalimbali wa mtaa wameaswa kutowapokea watu bila kuwa na barua za mahali walikotoka kwani iliwachukua muda ilikuzipata koo zote mbili kutokana na marehemu kuhamia mtaani hapo wiki mbili zilizopita.

Hata hivyo baada ya kushindwa kupatikana kwa muafaka balozi huyo wa mtaa Bwana Mwanyingili alitoa shilingi 25,000 kwa ajili ya kuupeleka mwili wa marehemu Hospitali ya rufaa Mbeya kusubiri maafikiano ya ndugu wa pande zote mbili waishio Nzovwe.

Tuesday, May 8, 2012

GEREZA LA RUJEWA LATEMBELEWA NA UMOJA WA WANAWAKE WA KANISA LA MOROVIAN.

Na Bosco Nyambege ,Rujewa
 Umoja wa Wanawake kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Magharibi katika Ushirika wa Yerusalemu iliyopo Mkoani Mbeya wamezuru Gereza la Rujewa iliyopo Wilayani Mbarali hivi karibuni.
 
Ziara hiyo iliambatana na kutoa zawadi kwawafungwa wote wa Gereza hilo kama katoni nane za sabuni,mafuta ya kujipaka yaani lotion na mafuta ya mgando dazani 40 ikiwa pamoja na chumvi .
 
Mwenyekiti wa umoja wa wanawake ushirika wa yerusalemu Eda Kapora alipohojiwa kuhusiana na suala hilo alidai kuwa hiyo ni moja ya huduma  wanayofanya wanawake amabyo ni dhamana ya mzigo wa liopewa na mwenyezi mungu wa kutembelea wajane  ikiwa pamoja na wafungwa ,watoto yatima  na watu wanaoishi katika mazingira magumu   .
 
Kapora aliongeza kuwa kwani mpaka sasa wamekwisha kutembelea vituo mbalimbali  kama vile watoto yatima ,nyumba za wajane  watu wanaoishi ktika mazingira magumu n a ka sasa wameanza kuzuru katika magereza .
 
Kwa upande wake mchungaji mlezi wa kanisa hilo Peter Mwambalaswa alisema kuwa dini iliyo safi n kutazama wafungwa  ,wajane  na wanaoishi katika mazingira magumu .
 
Hata hivyo alisema kuwa ni muhimu kwa kanisa lolote kutambua wajibu mkubwa waliopewa na mwenyezi mungu juu ya kuhudumia wale wanaowazunguka na wale walio mbali nao wanaohitaji msaada wao .
 
Vilevle alsema kuwa ni vyema askari magereza wanaofanya kazi ya kuwalinda wafungwa magerezani kutambua kwama wao ni wachungaji na mungu atawalipa kama watafanya yale wanaompendeza yeye .
 
 
Alison  Mwasile ambaye ni mchungaji wakanisa la Moravian Usharika wa Rujewa amewasihi wafungwa kuonesha ushirikiano wao mzuri baina  yao na mungu pindi wanapokuwa gerezani na pindi wanapokuwa wanatoka .
 
Mwasile alisema kuwa magerezani wapo walimu wazuri wa imanikwani hata kipindi cha yusufu alipfunga gerezani kuilikuwa na kusudi maalumu ambalo  mungu aliliweka  ndani yake .
 
Mmoja wa wafungwa amabaye jina lake hakutaka jina lake litajwe aliyaomba makanisa  na dini mbalimbali kuweza kuwaombea  kwani wapo walio magerezani hawana hatia  yeyote .
 
Kwa upande wake Askari wa Gereza hilo ambaye jina lake hakutaka litajwe katika gazeti hili alisema ujio wa makanisa  gerezani  kunapelekea wao kuona mwanga  katia maisha yao  kwani wanapata  mawazo mbalimbali  kutoka kwa watumishi wa mungu  kuhusiana na shughuli zao..
 
Alisema  kuwa  hata kwa  upande  wa wafungwa  ni furaha kubwa kuona watumishi wa mungu wanaokuja kuwatembelea maeneo hayo kwani  wanapata faraja  na matumani  katika  maisha  yao  hata wawapo  gerezani  .

TB Joshua Apigwa Stop Cameroon



The Cameroonian government has blacklisted Prophet Temitope Balogun Joshua of the Synagogue
Church of All Nations,
 
 saying that he is an agent of satan hoodwinking unsuspecting members of the public with “diabolical miracles”.

Cameroon Foreign Affairs Minister, Mr. Henri Eyebe Ayissi, in an officialcommuniqué he issued titled:“The Devil Is In the House”, described T.B. Joshua as a “son of the devil” pretending to be “a man of God.”

The minister warned hundreds of Cameroonians, trooping to Lagos, South West Nigeria, for miracles inJoshua’s church, to desist from taking the trip or face the consequences, as the country will not stand by them.
The communiqué written in French read in part:

“The Ministry of Foreign Affairs warns those who by naivety or deception of Emmanuel TV’s captivating images, or even thosewho by hopelessness, envisage taking the pilgrimage to Pastor T.B. Joshua’s Synagogue Church Of All Nations in Lagos, that they will do soat their own risk. 
 
The Cameroonian Government warns these pilgrims that they will face the consequences alone.This is motivated by the painful andshameful fact that Cameroonian men and women, in search of deliverance and blessings, once in that church, find themselves in bestial and pitiable conditions.

“Women are Molested; pilgrimsdispossessed of their belongings by armed robbers and left to sleep on the streets at the mercy of gangs. Many cases of assassinations haveeven been recorded. And this is without other cases that are not recorded at the Cameroonian Embassy in Lagos with the victims too ashamed to narrate their infernal odysseys once they are out of Hell,” the minister said.

The minister said that while the bible asks us to be discreet with gifts and donations to the poor, T.B. Joshua is seen daily dolling out bags of rice to indigent people.

It was learnt that hundreds of Cameroonians who sold their properties or borrowed money in the hope of getting miracles in T.B.Joshua’s Church, only got disappointed in Lagos.

It was also reported that Prophet TB Joshua’s TV station has gained popularity in Cameroon and many people are tempted to take the trip and receive healings and sudden blessings.

It says that Joshua is now in many households in Cameroon and many people believe the flashy images they watch on television

Saturday, May 5, 2012

Mstari Unaoniliza Kuliko Yote Katika Biblia – XVIII




Somo letu linaendelea. Katika mstari ule wa Luka 13:22 Biblia inaeleza kuhusu mtu mmoja aliyemuuliza Bwana Yesu kuhusu wingi wa watu wanaookolewa. Bwana Yesu akijibu swali hilo alisema kuwa JITAHIDINI KUINGIA KATIKA MLANGO ULIO MWEMBAMBA, KWA MAANA NAKWAMBIA KUWA WENGI WATATAKA KUINGIA LAKINI WASIWEZE. Pamoja na sababu nyingi ambazo nimekwisha kuzieleza katika masomo yaliyotangulia, leo katika Sehemu hii ya Kumi na Nane tunaendelea na sababu nyingine.

23. WATAKOSA MSINGI.
1Kor 3:10-11. “Kwa kadri ya Neema ya Mungu niliyopewa na Mungu, mimi kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake, lakini kila mtu aangalie anavyojenga juu yake. Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani YESU  KRISTO.”

Wapendwa, leo tutauangalia Msingi. Kila nyumba unayoiona ina msingi, na misingi imetofautiana, msingi wa nyumba ya kawaida ni tofauti na msingi wa ghorofa.  Msingi wa ghorofa Moja ni tofauti na msingi wa ghorofa Kumi. Jinsi  ghorofa linavyokwenda juu  ndivyo msingi unatakiwa kwenda chini, na ndivyo inatakiwa pia wajenzi kuchanganya material kwa kipimo kinachofaa, vinginevyo ghorofa hilo litaishia kuanguka.

Hapo juu tumesoma kuwa hakuna msingi mwingine nje ya Kristo. Maana yake ni hivi ILE SABABU ILIYOKUFANYA USEME UMEOKOKA NI MHIMU SANA SANA.

Wengine waliokoka kwa sababu walikuwa wagonjwa. Walipoambiwa sasa unatakiwa kuokoka, kwa kuwa anaumwa akasema sawa, si kwamba moyo wake ulimpenda Mungu kwa kweli. Wengine walikutwa gerezani, walipoambiwa habari ya kuokoka, na wakaambiwa, ukiokoka Mungu atakutoa jela, na kwa kuwa walikuwa wamebanwa iliwalazimu wakubali na kweli Mungu aliwafanyia hivyo. Wengine walisikia wahubiri wakisema wewe unayeteseka na umaskinu njoo kwa Yesu, atakupa kile na kile, na kwa kuwa walikuwa na hali mbaya wakalazimika kufanya hivyo, na si kwamba mioyo yao ilikuwa kweli imeamua kumfuata Bwana Yesu.

Utakumbuka siku moja Yesu aliwaambia watu waliokuwa wanamfuata kuwa, MSIKITENDEE KAZI CHAKULA  KINACHOHARIKA, AKASEMA MNANIFUATA KWA SABABU  MLIKULA MIKATE MKASHIBA. Mpendwa hebu jiulize: KWA NINI UNAMFUATA YESU?

Tuendelee na somo letu katika kuuangalia MSINGI.
Katika Ebr 6:1-6 kuna maneno ambayo nimeyapanga kama ifuatavyo:
“Kwa sababu hiyo tukiacha, kuyanena mafundisho ya kwanza,  ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu,
1. TUSIWEKE MSINGI TENA WA KUZITUBIA KAZI ZISIZO NA UHAI.
2. NA WA KUWA NA IMANI KWA MUNGU.
3. NA WA MAFUNDISHO YA MABATIZO.
4. NA KUWEKEA MIKONO.
5. NA KUFUFULIWA WAFU.
6. NA HUKUMU YA MILELE.
Ndugu zangu watoto wa Mungu, Maneno hayo hapo juu  ndiyo misingi ambayo kila aliyeokoka alitakiwa kufundishwa. Hiyo ndiyo itakufanya uendelee mbele. Hata kama wewe utakuwa ni ghorofa, hautaweza kuporomoka kamwe!
Sasa tutaendelea kuyapitia moja baada ya jingine ili uweze kuelewa vizuri. Ni ombi langu kuwa Mungu wetu aliyetuokoa atatupatia Neema ya kuweza kuelewa vizuri kwa uongozi wa Roho mtakatifu.

1.Kutubia kazi ambazo hazina uhai. Ni kitendo cha mtu  kutubu dhambi zake kwa mtu. Wengine wanaita Kuungama. Vyovyote utakavyoiita lakini tunapaswa kuungama dhambi zetu kwa YESU, na pia ni kuungama na kuziacha, kutozirudia tena.

Mith 28:13 “Afichaye dhambi zake, hatafanikiwa, bali aziungamaye na kuziacha atapata rehema”. Mpendwa Biblia inajieleza. Tunatakiwa tuziungama na kuziacha tofauti na mafudisho mafu kuwa mtu uende kanisani kila jumapili uungame dhambi kwa mtu. Jumapili hii utaungama kwake, na jumapili ijayo, na ile ijayo, mpaka mwezi, mpaka mwaka, unaanza tena mwaka mwingine! Hapana. Nenda kwa Yesu, ungama na kuziacha, utapata rehema.

Katika Yoh 9:31 tunaona kuwa Mungu hasikii wenye dhambi. Kama utaishi na dhambi, elewa kuwa Mungu hakusikii kabisa wakati unaomba. Atakusikia pale tu ukiziungama na kuziacha, tangu hapo atakuwa anakusikia.
Mith 8:13 “Kumcha Bwana ni kuchukia uovu.” Unajua wapendwa, kila mtu anasema “kweli namcha Mungu” au “nampenda Mungu”. Lakini sikia, jipime hapo katika mstari huo unasema kuwa KUMCHA MUNGU NI KUCHUKIA UOVU.

Hebu tuendelee kuona jinsi ya kuungama au kutubu: Ni kutokurudia yale ambayo mtu ameamua kuyaombea msamaha kwa Mungu. Yaani ni kumaanisha kile unachokisema.

Katika Yoh 5:10-14 kuna kisa cha mtu aliyekuwa amelala miaka 38, na wengine walikuwa wanaponywa maji yanapotibuliwa, ila yeye alikuwa haponywi. Siku moja Bwana wa huruma alimkuta amelala, akamuuliza kama anataka kuwa mzima nay eye akasema HANA MTU WA KUMTIA KWENYE BIRIKA.  Nafikiri hakuwa ameelewa swali. Kama wengi wetu tusivyoelewa wakati Bwana ansema na sisi. Utakumbuka Adamu aliulizwa kwa nini UMEKULA TUNDA? AKASEMA NI YULE MWANAMKE ULIYENIPA NDIYE AMENIPA TUNDA. Kumbe kama angeulizwa kuwa “ni nani amekupa tunda ukala?” ndipo angejibu hivyo. Pamoja na kutokujibu swali sawa sawa lakini Bwana akamwambia SIMAMA  JITWIKE GODORO LAKO UENDE. Naye akasimama akajitwika godoro akaenda. Mafarisayo walipomsumbua kuwa mbona amejitwika godoro wakati ilikuwa ni sabato yeye aliwajibu kuwa yule aliyemfanya awe mzima ndiye aliyemwambia ajitwike godoro!

Kama vile wengi wetu tukiishaokoka, watu huwa wanajitokeza kuulizia wokovu wetu, kuwa kwa nini hili, kwa nini umeacha dini yetu, kwa nini hili na lile. Ebu jibu liwe ni kwamba: “YEYE aliyenifanya mzima ndiye ameniambia nijitwike godoro
Yoh 5:14 “Baada ya hayo Yesu akamkuta ndani ya hekalu, akamwambia, angalia umekuwa mzima, usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi” 

Nimesema kutubu au kuungama ni kuacha, ni kugeuka upande mwingine, ni kuipa dhambi mgongo na kutokuirudia tena. Unaona Yesu alivyomwambia mtu huyu aliyekuwa amelala miaka 38, kuwa akirudia litampata baya zaidi ya hilo la kulala miaka 38. Je, ni lipi hilo baya zaidi?

Biblia inasema pepo akimtoka mtu hurudi tena, akikuta aliyemfukuza hayumo, huendea wengine SABA  walio wabaya zaidi ya yule, na hali ya mtu huyo huwa mbaya zaidi. Hayo yapo katika  Math 12:43

Katika Yoh 8:1-11 tunaona mwanamke mmoja aliletwa kwa Yesu, alikuwa amekamatwa kwenye zinaa, na wanawake wa namna ile walikuwa wanapigwa kwa mawe. Siku hiyo aliletwa kwa Yesu, na Yesu alimhurumia, akawaambia wale washtaki wake kuwa yeyote asiye na dhambi awe wa kwanza kumtupia jiwe, na wengine wafuate. Yule mwanamke alijua kuwa amekwisha, pengine alikuwa ameisha wahi kuona wengine wakipigwa kwa mawe, akawa anasubiri mawe. Biblia inasema Yesu akainama akawa anaandika chini, hatuelewi alikuwa anaandika nini, lakini wengine husema alikuwa anaandika dhambi ya kila mtu aliyekuwa pale, na kila mmoja alipoona vile, alikimbia. Mama yule alibaki peke yake na Bwana Yesu, na katika Yohana  8:10-11 “ Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia mwanamke, wako wapi washitaki wako?

2. Kuwa na Imani kwa Mungu. Ni kukubaliana na kile ambacho Neno  la Mungu linasema, hata kama kwa macho ya kibinadamu linaonekana kuwa haliwezekani kabisa. Ndiyo maana mtume Paulo akaandika kuwa: HATUENENDI KWA KUONA, BALI TUNAENENDA KWA IMANI. Hapo ndipo wanapopatikana au walipopatikana mashujaa wa Imani. Walikubaliana na Neno la Mungu bila kujali gharama. Wengine walikubaliana mpaka wakafa bila kubadilisha msimamo wao.
Ufunuo 2:10 “Usiogope mambo yatakayokupata, tazama ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani, ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.

Yuda 1:5 “Tena napenda kuwakumbusha, ijapokuwa mmekwisha kuyajua haya yote, ya kwamba Bwana akiisha kuwaokoa watu  katika Nchi ya Misri, aliwaangamiza baadaye wale wasoioamini”

Ndugu yangu, wakati mwingine shetani analaumiwa bure. Hapo juu unaona kuwa Bwana akiisha kukuokoa unapaswa kumwamini kuwa anaweza kabisa kukufikisha kule alikokuahidi. Haitakiwi kumtilia mashaka maana mashaka huletwa na uoga. Uoga ukiishaingia, hofu inaingia, mashaka naye anasogea, ndipo kutetemeka nako kunakuja kwenye mwili. Utakumbuka Mungu alimwambia Gidion, katika Waamuzi 7 hivi: “watu hawa walio pamoja nawe ni wengi mno hata nikawatie Wamidiani katika mikono yao, wasije Israel wakajivuna, juu yangu wakisema, mkono wangu mwenyewe, ndio ulioniokoa, basi sasa nenda  tangaza habari masikioni mwa watu hawa, na kusema  MTU AWAYE YOTE ANAYEOGOPA NA KUTETEMEKA, ARUDI AONDOKE KATIKA MLIMA  GILIADI. NDIPO WATU ISHIRINI NA MBILI ELFU WAKARUDI, KATIKA WATU HAO, WAKABAKI WATU ELFU KUMI.

Unaona! Mungu haendi na waoga, haendi na wanaotetemeka, hao ndio unasikia wanakufa na pressure, mishtuko. Ukiishaokoka hautakiwi kuwa hivyo. Elewa siku zote kuwa VITA SI VYAKO, ELEWA ALIYEMO NDANI YAKO NI MKUU KULIKO ALIYE KATIKA DUNIA, ELEWA  UNAYAWEZA MAMBO YOTE KATIKA YEYE AKUTIAYE NGUVU.

3. Mafundisho ya Mabatizo. Mpendwa, ninafundisha Misingi au Msingi wa Mkristo, ambao ukiishakuwa ndani yako hakuna kitakachokutikisa kamwe. Kumbuka Biblia inasema kuwa mwenye haki ni jasiri kama SIMBA. Ndiyo maana Bwana wetu Yesu anaitwa  SIMBA WA KABILA YA YUDA. Hata katika Biblia kuna Neno USIOGOPE  mara idadi ya siku za mwaka mzima. Kwa hiyo kila ukiamka asubuhi kuna neno “USIOGOPE” liko hapo kukusalimia.
Kwa nini Biblia inasema MABATIZO?     Haisemi UBATIZO, ni MABATIZO. Hii inaonyesha ni Mengi.

a). Ubatizo wa Maji. Katika Math 3:13 tunamwona Bwana wetu Yesu akienda Yordani kubatizwa. Yohana akambatiza akiwa mtu mzima tofauti na siku zetu unaona watu wanabatizwa wakiwa watoto wadogo, na wanatafuta mtu anakuwa baba yake wa ubatizo. Hiyo siyo Biblia.

Katika Mark 16:14 Biblia inasema AAMINIYE NA KUBATIZWA ATAOKOKA. Huyo anayebatizwa anatakiwa kuamini yeye mwenyewe kwa moyo wake, ndipo abatizwe. Kinyume cha hapo tunafundisha mambo yetu wenyewe, wala siyo ya Mungu.

Rumi 6:4 “Tulizikwa pamoja naye kwa njia ya UBATIZO”. Ubatizo ni ishara ya kuwa mtu amekufa, na anazikwa kwenye maji. Wapo wahubiri wengi wanasema haijalishi ni maji gani, yawe maji mengi au maji kidogo mradi umebatizwa. Mpendwa, ebu sikia maandiko haya hapa katika Math 24:4 “Yesu akajibu akawaambia ANGALIENI MTU ASIWADANGANYE”. Ni juu yangu, ni juu yako, ni juu ya kila mtu kuangalia asidanganywe. Atakayekubali kudanganywa basi atakapofika kwa Yesu, ataulizwa ilikuwaje ukafanya hivyo? Atasema nilidanganywa. Nakuambia ndugu yangu kuwa wala hakutakuwa na msamaha.

Kumbuka Mungu alimuuliza  ADAM “Kwa nini umekula tunda nililowakataza kwamba msilile?” Jibu: Mwanamke uliyenipa. ( Bado alipata adhabu}

HAWA naye akaulizwa: “Kwa nini umekula tunda?” Jibu: Nyoka alinidanganya nikala.  Pamoja na majibu hayo mazuri lakini bado hao wazazi wetu wa kwanza waliadhibiwa tu. Yule aliyepewa na mwanamke, na yule aliyedanganywa, wote waliadhibiwa!.

Hapo nilikuwa nazungumzia ubatizo wa maji mengi, maana kama Biblia inasema ni ishara ya mazishi, basi tuelewe kuwa mtu akifa huzikwa mwili mzima wala sio kichwa peke yake!

Nadhani utaniuliza swali kuwa, Sasa hao wanaobatiza watoto wadogo, wameyapata wapi hayo mafundisho? JIBU: Mark 7:6-7 “Akawaambia Isaya alitabiri vema, juu yenu enyi wanafiki, kama ilivyoandikwa, watu hawa huniheshimu kwa midomo, ila mioyo yao iko mbali nami, nao waniabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu”. Nakushauri kuwa kila unachofundishwa ebu kikague kama kweli kiko kwenye NENO la Mungu, yaani BIBLIA.

b). Ubatizo wa Roho Mtakatifu. Mdo 1:6-7 “Basi walipokutanika, wakamuuliza, wakisema; Je, Bwana wakati huu ndipo unapowarudishia Israel ufalme? Akawaambia siyo kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoweka katika mamlaka yake mwenyewe. Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilkia juu yenu Roho mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalem, na katika Uyahudi wote na Samaria na hata mwisho wa nchi” 

Roho ajapo ndani ya mtu ndiye humpa nguvu za kushinda maovu. Ndiye anakupa nguvu za kuwa shahidi.
Rumi 8:26. Hatujui kuomba ila Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa. Roho wa Mungu alikuwa ndani ya Yesu, ndiye huyo huyo akiwa ndani yako utaishi kama alivyoishi Yesu. Atakuombea kama alivyomwombea Yesu.

Ebr 5:7 “Yeye siku hizo za mwili wake, alimtolea yule awezaye kumwokoa na kumtoa katika, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu”. Mpendwa, kama Yesu ndivyo aliishi duniani, kwa kilio kikuu, naye alisaidiwa na Roho Mtakatifu, basi mimi na wewe kama tunataka tushinde tunamhitaji Roho mtakatifu, ndiye atakaye tusaidia.

Gal 4:6 “Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanae  mioyoni mwetu, aliaye ABA yaani Baba”. Ndugu yangu pengine umeokoka, au hujaokoka, Ubatizo wa Roho mtakatifu ni muhimu sana katika maisha ya Mkristo, na huyo ndiye ataendelea kukufundisha Neno la Mungu na kukuweka kwenye kweli yote.

c). Ubatizo wa Mateso. Luka 12:49-53. “Nimekuja kutupa moto duniani, na ukiwa umeishawashwa, ni nini nitakalo zaidi, lakini nina ubatizo unipasao kubatizwa, nami nina dhiki kama nini hata utimizwe. Je, mwadhani ya kwamba nimekuja kuleta amani duniani? Nawaambia la sivyo bali mafarakano. Kwa kuwa tokea sasa katika nyumba moja, watakuwamo watu watano wamefarakana, watatu wa kwa wawili, wawili kwa watatu. Watafarakana baba na mwanawe, mwana na baba yake, mama na binti yake na binti na mamaye, mkwe mtu na mkwewe, mkwe na mkwe mtu”

Hayo yote yanaeleza jinsi safari ya Mbinguni inavyomkabili mtu peke yake bila kutegemeana. Kwa hiyo unatakiwa uiangalie Biblia inachokufundisha, kishike, kikumbatie. Wengine wanasema baba kanizuia kuokoka, mama kanizuia kuokoka, kaka, au baba mkwe. Hapana! Kila mtu atasimama mbele za Bwana atoe habari zake mwenyewe.
Bwana akasema anao ubatizo mwingine ambao ni shida kama nini kuutimiz!. Ndugu zangu, Yesu alikuja akatuachia kielelezo hapa duniani. Yaliyompata ndio yatatupata. Kama watu walimpenda, basi watatupenda tu na sisi, kama walimchukia ebu tujue kuwa yaliyompata ndiyo yatatupata. Ndio maana alisema mtu akitaka kumfuata AUBEBE MSALABA WAKE AMFUATE. Kumbuka MSALABA maana yake ni MATESO.

Ni kweli kwamba hatuwezi kusulubiwa kama alivyosulubiwa, ila tunasulubiwa kwa namna moja au nyingine.
Mdo 14:21-22. “Hata walipokwisha kuihubiri Injili katika mji ule, na kupata wanafunzi wengi, wakarejea mpaka Listra, na Ikonio, na Antiokia (yafuatayo nimeyapanga mwenyewe kuwa):
    i. WAKIFANYA IMARA ROHO ZA WANAFUNZI.
    ii. WAKIWAONYA WAKAE KATIKA ILE IMANI.
   iii.WAKIWATAARIFU KUWA TUMEPASWA KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU KWA NJIA YA DHIKI NYINGI.
Ndugu zangu wapendwa, kusudi la Injili ya Kristo tunayoihubiri  linatakiwa  kuwa katika sehemu hizo 3.

Kufanya roho za wanafunzi kuwa imara. Kwa nini zifanywe Imara? Kwa kuwa baada ya kuokoka huwa tunakutana na mambo mazito kiasi kwamba kama mioyo yetu haiko imara kwa Neno la Mungu, hatuwezi kufika popote. Tutaishia kusema tu nimeokoka, lakini mwisho wa siku, unakuta moyo huo ambao haukufanywa imara umebomoka. Ndio maana kwenye milango yetu tunaweka makomeo, na tukiisha funga twaweza kulala. Na mioyo yetu inatakiwa kufanywa Imara. Ndiyo maana imeandikwa katika Mith 4:23 kuwa “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo, maana huko ndiko zitokazo chemi chemi za uzima”. Na moyo unalindwa kwa NENO la Mungu. Ndiyo maana imeandikwa kuwa NENO LA KRISTO LIKAE KWA WINGI NDANI YETU.

Kazi ya 3: Kuwataarifu kuwa kuingia mbinguni ni kwa njia ya dhiki nyingi. Ndugu yangu, Biblia vile ilivyoandikwa ndivyo ilivyo. Hatupaswi kuigeuza, wala kuichakachua, au kuigoshi, imeeleza wazi wazi kuwa tutaingia kwa njia ya DHIKI NYINGI. Pata muda soma vizuri Neno katika kitabu cha MASHUJAA WA IMANI, cha Waebrania sura ile ya 11.

1Pt 2:18-23. “Enyi watumishi, watiini bwana zenu, kwa hofu nyingi, sio wao walio wema na wapole tu, bali nao walio wakali, maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki, kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi. Lakini kustahimili mtendapo MEMA NA KUPATA MATESO, huu ndio wema hasa mbele za Mungu, maana ndiyo mlioitiwa, maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo mfuate nyayo zake. Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake, yeye alipotukanwa hakurudisha matukano, alipoteswa, hakuogofya, bali alijikabidhi kwake ahukumuye kwa haki”.

Ndugu yangu, ebu soma hayo maandiko hapo juu. Mimi na wewe tujipime kwake huyo ambaye tunaambiwa tufuate nyayo zake. Je, tunazikanyaga nyayo zake kweli? Au zetu zimepanuka? Au zimepwaya?

2Timotheo 3:10-12. “Bali wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, makusudi yangu, na Imani na uvumilivu, na upendo na saburi, tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonia, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote. Naam na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa wataudhiwa.”

Mistari hiyo inatuonyesha jinsi watumishi wa kweli walivyoishi, ambao Biblia inasema wazi wazi  kuwa TUMEJENGWA KATIKA MSINGI WA MITUME NA MANABII. Kwa kusema hivyo ni kwamba njia waliyoipitia ndiyo tutaipitia, ambayo ndiyo ile  Bwana wetu Yesu aliipitia. Ndio maana walikuwa wakipita na kuwajulisha kuwa wakae wakijua kuwa TUTAINGIA KWA NJIA YA DHIKI NYINGI.

Ndugu zangu leo nitaishia hapa katika sehemu hii ya Kumi na Nane. Misingi mingine iliyobakia, ambayo ni Kuwekea Mikono, Kufufuliwa Wafu na Hukumu ya Milele nitaielezea katika Sehemu ifuatayo ya Kumi na Tisa.

Ndugu mpendwa, ninakushauri kuwa baada ya kusoma Misingi hiyo niliyoielezea jikite katika kuitafakari na kuitendea kazi ili roho yako ipate kuwa imara katika safari hii, kwa maana ya kwamba dhiki zitakapokuja wala usishangae, na uwe na uwezo wa kupita na upate kuitwa MSHINDI!
Ubarikiwe na Bwana.
Ndugu yenu Mchungaji Samuel  Imori.

KONGAMANO LA KUOMBEA MKOA WA MBEYA DHIDI YA VITENDO VIOVU KUFANYIKA MEI 5 MWAKA HUU.

Mbunge wa Viti Maalum wa Mkoa wa Mbeya mheshimiwa Dakta Mary Mwanjelwa  mbunge wa viti maalum mkoa wa mbeya akiongea na wananchi wa mwanjelwa  katika kiwanja cha sido, ambaye anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi katika Kongamano la Maombi la kuuombea Mkoa dhidi ya Vitendo viovu.
*****
 Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Kongamano la Maombi ya kuuombea Mkoa wa Mbeya, dhidi ya vitendo viovu vikiwemo vya upigaji nondo, kujichukulia sheria mkononi, uchunaji ngozi, mauaji ya albino, watoto na imani za kishirikina litafanyika leo katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari St Mary iliyopo Forest mpya jijini Mbeya.

Mgeni rasmi katika Kongamano hilo anatarajiwa kuwa Mbunge wa viti Maalumu wa Mkoa wa Mbeya Dakta Mary Mwanjelwa, ambapo atafuatana na viongozi mbalimbali wa Serikali mkoani hapa.

Kongamano hilo limeratibiwa na Kipindi cha Faraja yako kinachorushwa kila siku kuanzia saa 11:00 alifajiri mpaka 12:30 asubuhi na saa 3:00 usiku mpaka 4:00 usiku katika kituo cha Kurushia matangazo cha Bomba FM redio, kupitia masafa ya 104.0 kilichopo mkoani hapa.

Aidha, baadhi ya vitendo vilivyotokea hivi karibuni mkoani hapa ni pamoja na kupingwa nondo Muimbaji wa nyimbo za Injili nchini Bwana Medrick Sanga, Aprili 10 mwaka huu wakati akienda katika studio za kurekodi muziki maarufu kwa jina la Mbeya Records iliyopo ndani ya Kanisa la KKKT Usharika wa Forest.

Hata hivyo mbali na tukio hilo watu kadhaa wamedaiwa kuuawa kwa imani za kishirikina na mwingina kuzikwa hai baada ya kuhusishwa kuwa ni mchawi na pia watoto wa shule kuanguka mara kwa mara wawapo mashuleni kwao.

ASKOFU ANILIKISA CHEYO AWATAKA WAKRISTO KUJIENDELEZA KIELIMU.

Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho Bwana David Mwankina (kushoto), akifuatiwa na Askofu wa Kanisa la Moravian Tanzania Alinikisa Cheyo, Mgeni rasmi Dr Victoria Kanama na Mkuu wa Chuo hicho cha Ualimu Eliackim Mtawa.
*****
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Askofu kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania Alinikisa Cheyo, amewataka waumini kuthamini elimu ili kuleta tija katika jamii.

Ameyasema hayo alipokuwa akifungua maombi kwenye Chuo cha Ualimu cha Kanisa la Moravian Mbeya katika mahafali ya pili ya chuo hicho Mei 3 mwaka huu jijini Mbeya.

Akinukuu baadhi ya vifungu katika biblia Askofu Cheyo amesema wazazi na walezi wanapaswa kuwajengea msingi wa elimu vijana kwani ndio urithi utakao wasaidia maishani mwao, badala ya mali kwani mali huisha au kupotea.

Kwa upande wake mgeni rasmi Dr Victoria Kanama, ambaye ni Mkurugenzi wa Hospitali ya K'S iliyopo jijini hapa na pia ni Mkuu wa Bodi ya Chuo Kikuu cha TEKU, amewataka wahitimu kufuata maadili mazuri ya ualimu na hivyo kuwa mabalozi wazuri wa chuo hicho, ambapo pia alikazia suala la kujiendeleza kielimu zaidi na kutobweteka.